STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 7 Desemba 2014

Ronaldo afikisha mabao 200, sasa kinara wa hat trick La Liga






Cristiano Ronaldo celebrates his clinical hat-trick that sent records tumbling during a 3-0 victory at the Bernabeu
Ronaldo alishangilia moja ya mabao yake jana
Cristiano Ronaldo
Akiendelea kufunga
Cristiano Ronaldo
jamaa huyu balaa!
Real Madrid v Celta Vigo
Akishangilia na wenzake ushindi wa nyumbani Santiago Bernabeu
MWANASOKA Bora Duniani, Cristiano Ronaldo usiku wa jana alifikisha bao lake la 200 katika Ligi Kuu ya Hispania, baada ya kupiga 'hat trick' wakati Real Madrid ikiiangamiza 'Celta Vigo kwa mabao 3-0 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Hat trick hiyo ni ya 23 kwa Mreno huyo na kumfanya kuwa mchezaji anayeongoza kwa hat trick nyingi katika La Liga kwa sasa, licha ya kukamata nafasi ya 9 ya wachezaji wenye magoli mengi katika ligi hiyo akiwa nyuma ya mabao 53 dhidi ya  'hasimu' wake, Lionel Messi mwenye mabao 253.
Mabao hayo yamemfanya mchezaji huyo kufikisha mabao 200 katika mechi 178 za La Liga kwa misimu wake wa sita nchini humo na pia ni bao la 23 katika mechi 13 za msimu huu, kiasi ambacho ukichukua mabao ya hasimu wake na ya mshambuliaji mwingine nyota wa Barecelona, Neymar hayafikii idadi hiyo ya mabao.

Ronaldo ambaye hakuwepo katika mechi ya Kombe la Mfalme wakati Real Ikishinda mabao 5-0 dhidi ya Cornellà, alianza kuandika bao la kwanza kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 36.
Katika kipindi cha pili mkali huyo aliongeza tena mabao mawili katika dakika ya 65 na na 81 alipomaliza kazi nzuri ya Marcelo na kuifanya Real kuzidi kujichimbia kileleni na kuikimbia Atletico.
Ushindi huo umeifanya Real kufikisha pointi 36 wakati wapinzani wao ambao pia ndio mabingwa watetezi wakiwa na 32.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo jana Athletico Bilbao ililala nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Cordoba na leo kutakuiwa na michezo mingine kadhaa likiwamo pambano la Barcelona dhidi ya wapinzani wao wa Jimbo la Cataluna, Espaniola.
Real Madrid: Casillas; Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo; Rodriguez (Arbeloa 53mins), Illarramendi, Kroos; Bale, Benzema (Coentrao 81'), Ronaldo (Hernandez 85')
Booked: Rodriguez, Carvajal, Arbeloa, Illarramendi
Goals: Ronaldo (pen) 36' 65' 81'

Celta Vigo: Sergio; Mallo, Cabral (Gomez 74'), Fontas, Jonny; Radoja, Hernandez, Krohn-Dehli (Mina 82'); Orellana (Fernandez 69'), Nolito, Larrivey
Booked: Cabral, Jonny, Nolito, Hernandez
Wakali wa Hat Trick wa Muda wote La Liga Hawa Hapa:
23- CRISTIANO RONALDO 
22- Di Stéfano and Zarra 
20- Messi
19- Mundo 
16- César
13 Lángara

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox