Kocha
wa timu ya taifa ya Brazil Carlos Dunga amemuita beki wa Arsenal
Gabriel Paulista katika kikosi chake kitakachocheza mechi ya kirafiki
dhidi ya Ufaransa na Chile mwishoni mwa mwezi huu.
Paulista
amepata nafasi hiyo kwa mara ya kwanza baada ya Dunga kufanya
mabadiliko ya wachezaji watatu katika kikosi chake kufuatia kuumia kwa
mabeki watatu, David Luiz,Diego Tardeli na Marquinhos.
Beki
huyo wa kati aliyesajiliwa mwezi januari mwaka huu akitokea Villarreal
ameshaichezea klabu ya Arsenal Mechi nne mpaka sasa.
Luiz
alipata maumivu ya nyuma mguu katika mechi ya wiki iliyopita
waliyofungwa na Bordeaux huku Marquinhos akisumbuliwa na matatizo ya
kubwana na misuli.
Kikosi
hicho cha Brazil kitakutana siku ya jumatatu au jumanne mjini Paris
tayari kwa maandalizi ya mechi ya alhamisi dhidi ya Ufaransa katika
dimba la Parc des Princes
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni