Watu wa soka wana mambo yao. Sasa wameibuka
na mpya kwamba mguu wa mshambuliaji nyota wa Barcelona, Lionel Messi una
ubongo.
Picha ya kibonzo kikionyesha Messi akipimwa
na profesa mmoja imezua gumzo mitandaoni.
Hii ni katika kuonyesha kukubaliana na
kiwango cha juu alichokionyesha Messi wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
dhidi ya Manchester City, jana.
Messi alikuwa moto wa kuotea mbali na kuiongoza Barcelona kushinda kwa bao 1-0 na kujihakikisha nafasi katika robo fainali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni