MWENYEKITI wa Chama cha
Soka cha Uingereza-FA Greg Dyke anapanga kuzungumza na kocha wa timu ya
taifa ya nchi hiyo Roy Hodgson kuhusu mkataba mpya mapema mwaka
ujao. Hodgson mwenye umri wa miaka 67 alichukua mikoba ya Fabio Capello
Mei mwaka 2012 lakini kikosi chake kilijikuta kiking’olewa katika hatua
ya makundi ya Kombe la Dunia mwaka jana. Hata hivyo, Uingereza ndio
wanaoongoza kundi lao katika mechi za kufuzu michuano ya Ulaya mwakani
baada ya kushinda mechi zao nne za kwanza. Mkataba wa sasa wa Hodgson
unamalizika baada ya michuano ya Ulaya itakayofanyika nchini Ufaransa na
Dyke amesema mapema mwakani watajadiliana kuhusiana na mustakabali wa
kocha huyo. Hodgson ambaye amewahi kuinoa Switzerland kuanzia mwaka 1992
mpaka 1995, aliiwezesha Uingereza kutinga hatua ya robo fainali ya
michuano ya Ulaya mwaka 2012 ambapo walitolewa kwa changamoto ya mikwaju
ya penati na Italia.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 26 Machi 2015
FA KUMUONGEZA MKATABA HODGSON MWAKANI.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni