MCHEZO wa fainali ya
Kombe la Mfalme kati ya Athletic Bilbao na Barcelona unaotarajiwa
kuchezwa Mei 30 mwaka huu, utafanyika katika Uwanja wa Camp Nou. Kwa
kawaida fainali ya michuano hiyo hufanyika katika uwanja huru lakini
kutokana na klabu ya Real Madrid kukataa kutumika kwa uwanja wake wa
Santiago Bernabeu kuliamuliwa kupigwa kura katika mkutano na Shirikisho
la Soka la Hispania. Hakuna timu yeyote iliyotumia katika uwanja wake
katika mchezo wa fainali toka mwaka 2002 wakati Deportivo La Coruna
walipoifunga Real Madrid katika uwanja wao. Katika mkutano huo viwanja
vya Vicente Calderon wa Sevilla na Mestalla wa Valencia vyote vilikuwa
vikitafuta nafasi ya kuandaa fainali hiyo lakini waliondolewa katika
duru la kwanza la kura na kubaki na Camp Nou pamoja na Uwanja wa San
Mames wa Bilbao. Ushindi katika mchezo huo utaifanya Barcelona kufikisha
mataji 27 ya michuano hiyo, wakati Bilbao wao wako katika nafasi ya
pili katika orodha kwa kufikisha mataji 23 kama wakishinda.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 26 Machi 2015
KOMBE LA MFALME KUFANYIKA KATIKA UWANJA WA CAMP NOU.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni