Mchezaji wa mieleke maarufu nchini Mexico, Hijo del Perro Aguayo, amefariki dunia wakati alipodondoka jukwani ikiwa ni saa chache baada ya kukimbizwa hospitali.
Mwanamieleka huyo alikuwa akipigana na mwezake Rey Mysterio, katika pambano lililofanyika ijumaa usiku na mara baada ya kudondoka alikimbizwa hospitali lakini madaktari walithibitisha kuwa tayari amefariki.
Wakati akiwa amedondoka chini wenzake hawakujua kiasi gani ameumia na kuendelea na mchezo na baada ya dakika zipatazo mbili waligundua kuwa amezidiwa hivyo kumuwahisha hospitali.
Hata hivyo uchunguzi kuhusiana na uwezekano wa kuua bila kukusudia umefunguliwa baada ya mtoto wa ncheza mieleka maarufu kufariki dunia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni