Kiungo
wa klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ujerumani Mesut Ozil amesema
miaka ijayo anaamini atashinda tuzo ya Ballon d'or na jinsi wachambuzi
wanavyozidi kumkosoa ndiyo anapata nguvu ya kujituma zaidi.
Mjerumani
huyo ameichezea Arsenal mechi 14 tu katika ligi kuu msimu huu kufuatia
kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza majeraha lakini tangu arudi
tena uwanjani amekuwa katika kiwango bora.
Mchezaji
huyo aliyesajiliwa msimu uliopita akitokea Real Madrid anaonekana
kuizoea ligi ya Uingereza tofauti na hapo awali. "Nikiendelea kufanya
vizuri, afya yangu ikawa imara basi miaka michache ijayo Ballon d'or
itakuwa mikononi mwangu" alisema Ozil. ."Ninajisikia vizuri. Mimi ni
mchezaji mkubwa duniani,ninacheza katika klabu kubwa. Pia hii ligi
tunatumia nguvu nyingi kuliko kule La Liga kwa hiyo ninazidi kuimarika
zaidi kuliko mwanzo " aliongeza Ozil.
Pia
mchezaji huyo amesema kitendo cha kiungo wa zamani wa Manchester United
Paul Scholes kuponda kiwango chake kilimuongezea nguvu ya kupambana na
kuongeza kujituma zaidi.
Ozil
sasa yupo katika majukumu ya timu ya taifa ya Ujerumani ambao jumapili
watashuka dimbani kuwavaa Georgia katika mechi ya kutafuta tiketi ya
kufuzu michuano ya mataifa Ulaya yatakayofanyika mwaka 2016 nchini
Ufaransa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni