KOCHA wa timu ya taifa
ya Ujerumani, Joachim Loew amedai kuwa kikosi chake kilishindwa kutumia
mfumo wao wakati walipotoa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Australia katika
mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika jana. Katika mchezo huo
mabingwa hao wa dunia ndio waliotangulia kupata bao la kuongoza kupitia
kwa Marco Reus kabla ya Australia kusawazisha na kuongeza bao kupitia
kwa Mile Jedinak na James Troisi. Mshambuliaji Lukas Podolski aliyeingia
akitokea benchi aliisawazishia Ujerumani bao katika dakika ya 81 ya
mchezo na kupelekea timu hizo kutoshana nguvu katika mchezo
huo. Akihojiwa kuhusiana na mchezo huo, Loew anadhani kikosi chake
kilishindwa kuendeleza mipango na aina ya uchezaji walioanza nao katika
kipindi cha kwanza. Kocha huyo amesema mwanzoni walitengeneza nafasi
nyingi lakini walishindwa kabisa kucheza mchezo wao katika kipindi cha
pili hivyo kupelekea mchezo kuwaelemea.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 26 Machi 2015
SARE YAMPA WASIWASI LOEW.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni