STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 26 Machi 2015

SARE YAMPA WASIWASI LOEW.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Loew amedai kuwa kikosi chake kilishindwa kutumia mfumo wao wakati walipotoa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Australia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika jana. Katika mchezo huo mabingwa hao wa dunia ndio waliotangulia kupata bao la kuongoza kupitia kwa Marco Reus kabla ya Australia kusawazisha na kuongeza bao kupitia kwa Mile Jedinak na James Troisi. Mshambuliaji Lukas Podolski aliyeingia akitokea benchi aliisawazishia Ujerumani bao katika dakika ya 81 ya mchezo na kupelekea timu hizo kutoshana nguvu katika mchezo huo. Akihojiwa kuhusiana na mchezo huo, Loew anadhani kikosi chake kilishindwa kuendeleza mipango na aina ya uchezaji walioanza nao katika kipindi cha kwanza. Kocha huyo amesema mwanzoni walitengeneza nafasi nyingi lakini walishindwa kabisa kucheza mchezo wao katika kipindi cha pili hivyo kupelekea mchezo kuwaelemea.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox