MENEJA wa klabu ya
Arsenal, Arsene Wenger amesema sheria ya mabao ya ugenini inapaswa
kutumika baada ya muda wa nyongeza kuliko katika muda wa kawaida kama
ilivyo sasa. Arsenal walienguliwa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa
Ulaya kwa sheria ya bao la ugenini baada ya kutoka sare ya mabao 3-3
dhidi ya Monaco ya Ufaransa. Timu hiyo ilipoteza mchezo wao wa kwanza
kwa kufungwa mabao 3-1 Februari 25 mwaka huu kabla ya kujirudi na
kuifunga Monaco mabao 2-0 katika mchezo wao wa maridiano uliofanyika
katika Uwanja wa Louis 11 na Monaco. Wenger amesema sheria hiyo ilitungwa
katika miaka ya sitini na uzito wa bao la ugenini hivi sasa ni
mkubwa. Bao la ugenini huwa linahesabika baada ya muda wa nyongeza
katika mechi za mkondo wa pili kwenye michuano ya Kombe la Ligi hatua ya
nusu fainali lakini kwa upande wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na Europa
League sheria hiyo hutumika baada ya muda wa kawaida wa dakika 90
kumalizika. Wenger amesema timu mbili za Uingereza zimeondolewa katika
michuano hiyo kwa sheria ya bao la ugenini jambo ambalo wahusika
wanapaswa kujiuliza nap engine kuangalia upya sheria hiyo. Kocha huyo
aliendelea kudai kuwa wakati sheria hiyo ikitungwa katika miaka ya
sitini ilikuwa na dhumuni ya kuzifanya timu kushambuliana lakini soka
hivi sasa limebadilika.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumamosi, 21 Machi 2015
WENGER ATAKA SHERIA YA BAO UGENINI KUBADILISHWA.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni