STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 1 Aprili 2015

Beki wa Simba atimka kikosini kisa nyumba na pesa


Mlinzi wa kulia wa klabu ya Simba Hassan Kessy ametimka kwenye kikosi cha timu hiyo baada ya kushindwa kumpa nyumba na pesa anazodai
Mlinzi wa kulia wa klabu ya Simba Hassan Kessy ametimka kwenye kikosi cha timu hiyo baada ya kushindwa kumpa nyumba na pesa anazodai
Beki wa kulia wa ‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba Hassan Kessy ametimka kikosini na kuelekea nyumbani kwao Morogoro baada ya uongozi wa klabu hiyo ya Msimbazi kushindwa kumtafutia nyumba ya kuishi.
Kessy amesema kuwa, katika makubaliano yake na Simba walimuahidi wangempa nyumba ya kuishi lakini hali imekua tofauti kwani amekua akiishi kama ‘njiwa’ na uongozi hauonekani kujali. Amesema mbaya zaidi ni pale wachezaji wengine wanapoonekana ni muhimu kwenye klabu na kujaliwa kuliko wengine.
“Simba waliniahidi wangenitafutia nyumba, lakini toka nimekuja Dar es Salaam nimekuwa nikikaa kwa watu tu, mara leo hapa kesho pale. Nataka niwe na sehemu ya kupumzika, nikitoka kazini narudi nymbani kwangu, lakini Simba wameshindwa kutekeleza hilo, amesema Kessy.
“Nimeamua kurudi nyumbani Morogoro hadi hapo mambo yatakapokuwa sawa, nikihakikishiwa nyumba na pesa yangu nayodai nitarejea kuendelea na kazi. Mpira ni kazi yangu, sasa kama watu wanakuwa hawajali kazi yangu siwezi kuwaelewa,” ameongeza Kessy.
Meneja wa mchezaji huyo Athumani Tipo amesema, Simba walikubali kumtafutia Kessy nyumba ya kuishi lakini imekuwa tofauti, na kila anapowatafuta viongozi wa timu ili kutaka kujua hatma ya mchezaji huyo wamekuwa hawapokei simu yake.
“Simba walikubali kumtafutia Kessy nyumba ya kuishi lakini toka amejiunga na kikosi hicho mambo yamekuwa tofauti, amekuwa anaishi kwa watu hadi ameamua kurudi nyumbani mpaka hapo tutakapoweka mambo sawa. Lakini pindi napowatafuta viongozi wa Simba ili kujua tutalitatua vipi suala hili wamekuwa hawapokei simu zangu na kuleta ‘ujanjaujanja’” amesema Tipo.
Afisa habari wa Simba Haji Manara yeye amesema mchezaji huyo hayupo kwenye kikosi kutokana na matatizo ya kifamilia, lakini alipobanwa zaidi akasema hakuna mtu anayejua mkataba wa Kessy na Simba ukoje hivyo inawezekana malalamiko ya Kessy yakawa hayapo kwenye mkataba.
Leo kikosi cha Simba kimesafiri kuelekea Shinyanga kwa ajili ya mchezo wake dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa Jumamosi kwenye uwanja wa CCM Kambarage lakini Kessy hayupo kwenye kikosi kilichosafiri leo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox