Kiungo mkabaji wa klabu ya Simba SC, Jonas Mkude amefiwa na baba yake mzazi mzee Gerrad Mkude aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.
Juzi akiwa mjini Shinyanga ambako kikosi chake kipo huko kwa ajili ya mechi dhidi ya Kagera Sugar, Mkude alipigiwa simu kutoka nyumbani kwao Kinondoni, Dar es salaam na kupewa taarifa kuwa, baba yake amezidiwa sana na baadae akafariki dunia.
Hili ni pigo kubwa kwa Mkude kwani baba yake bado alikuwa anahitaji kula matunda ya mwanae wa kumzaa aliyejaaliwa kipaji kikubwa cha soka.
Mkali huyo wa Msimbazi tayari ameshaondoka Shinyanga na kurejea nyumani kwao Kinondoni, Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za mazishi ya baba yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni