Meneja wa Chelsea ,Jose Mourinho alimtukana tusi kubwa Daktari wa klabu hiyo, Eva Carneiro.
Video
iliochiwa na Sky Sports imeonesha Mourinho alivyomchukia na kumtukana
Eva kwa maneno ya kireno ‘filho da puta’ (ambayo tafsiri yake ni mtoto
wa mbwa).
Chanzo
cha Mourinho kumtukana Carneiro ni kuingia uwanjani kumtibu Eden
Hazard wakati wa dakika za majeruhi za mechi ya Jumamosi iliyopita dhidi
ya Swansea ambayo walitoka sare ya 2-2 uwanja wa Stamford Bridge .
Sportsmail
nao wanasema wachezaji wa Chelsea wameduwaa na maneno makali ambayo
Mourinho anabwatukajuu yao na viongozi wengine wa timu.
Mourinho
leo anakutana na vyombo vya habari kwa mara ya kwanza tangu
amtukane Carneiro na kumfungia kukaa kwenye bechi katika mechi zijazo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni