Neymar amemtaja Sergio Ramos kuwa ni moja ya mabeki visiki kabisa aliowahi kukutana nao katika maisha yake ya soka.
Nyota
huyo wa Barcelona amemuelezea mlinzi huyo wa kati wa Real Madrid kama "
beki kisiki" wakati alipokuwa akiulizwa ni beki gani ambaye anahisi
humletea shida katika maisha yake ya soka.
Lakini
hata hivyo Neymar pia amesema wachezaji wenzake Javier Mascherano na
Gerard Pique pia humpa shida wakati wakiwa mazoezini bila ya kusahau
Mbrazil mwenzake Thiago Silva.
"Ni
vigumu kusema kuhusu hili, kuna mabeki wengi sana wa kiwango cha juu"
alisema. "wapo kina Mascherano, Pique, Thiago Silva ila Sergio Ramos -
ni beki wa kati bora sana".
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni