STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 13 Agosti 2015

LEHMANN AZUNGUMZIA SAKATA LA CECH KUFUATIA KURUHUSU MAGOLI YA KIZEMBE MCHEZO WA WEST HAM


Nguli wa Arsenal Jens Lehmann amemsisitiza Petr Cech kufurahia msimu bora kabisa katika klabu ya Arsenal, lakini amemuasa kuwa anahitaji muda kuweza kuzoea maisha mapya klabuni hapo kufuatia uhamisho wake kutoka Chelsea.

Cech alifanya makosa ya kizembe ambayo yaliigharimu Arsenal kupoteza mchezo wake wa kwanza wa ligi kwa mabao 2-0 dhidi ya West Ham uliopigwa Jumapili katika dimba la Emirates huku ukiwa ndio mchezo wake kwanza wa ligi akiwa ndani ya uzi wa Arsenal.

Lehmann, ambaye alikuwa katikati ya lango katika kikosi cha Arsenal kilichotwaa ndoo ya EPL bila ya kufungwa msimu wa 2004, amekiri kushtushwa na kiwango cha Cech lakini anaamini kwamba mlinda mlango huyo atakuja kivingine na kuonesha yale aliyokuwa akiyafanya pindi alipokuwa Chelsea.

"Nimeshangazwa kwa sababu nilitarajia kuona akionesha kiwango kikubwa punde tu msimu unapoanza”, Lehmann alikaririwa na mtandao wa Goal kutoka Marekani.

"Lakini wakati mwingine inachua muda kidogo kuzoea mazingira mapya, hasa unapotoka kwa mahasimu wako wakubwa kama Chelsea. Huchukua muda kwa kweli, cha msingi anatakiwa kusahau yote hayo.



"Ni aina ya makipa ambao Arsenal walikuwa wakihitaji ili kutwaa ubingwa", Lehmann aliongeza. "Ana uzoefu wa kutosha, yaani ana sifa zote za kuwa mlinda mlango bora na naweza kusema ni miongoni mwa walinda mlango bora kabisa ulimwenguni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox