Fernando
Torres amezidi kumpa nguvu Mhisapaniola mwenzake Pedro, kuwa atapata
mafanikio makubwa endapo ataelekea kucheza ligi kuu nchini Uingereza.
Hali
hiyo imetokana na tetesi kuwa Pedro yuko mbioni kujiunga na Manchester
United akitokea klabu ya Barcelona, huku fununu nyingine zikieleza kuwa
tayari miamba hiyo imeshafikia makubaliano ya ada ya mwanzo ya uhamisho
ya pauni milioni18.1 na nyongeza(bonus) ya pauni milioni 4.2 endapo
mchezaji huyo atafanya mambo makubwa zaidi.
Torres,
ambaye amecheza EPL kwa takribani miaka 7 akiwa na Liverpoo na baadaye
Chelsea, amesisitiza kuwa Pedro ana uwezo wa kucheza England hasa
ikizingatiwa anataka nafasi zaidi ya kucheza.
“Ni rafiki yangu sana, na endapo ataamua kuelekea Uingereza, basi naamini atafanya vizuri tu”. Torres aliliambia Daily Mirror.
“Ana
sifa zote za kukipiga EPL, amekuwa Barcelona kwa miaka mingi sana,
hivyo naamini ana uwezo mkubwa ukiongezea pia na nidhamu ya uwajibikaji
wake uwanjani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni