STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 13 Agosti 2015

TORRES AMJUZA PEDRO JUU YA KUTIMKIA LIGI KUU NCHINI UINGEREZA.....


Fernando Torres amezidi kumpa nguvu Mhisapaniola mwenzake Pedro, kuwa atapata mafanikio makubwa endapo ataelekea kucheza ligi kuu nchini Uingereza.

Hali hiyo imetokana na tetesi kuwa Pedro yuko mbioni kujiunga na Manchester United akitokea klabu ya Barcelona, huku fununu nyingine zikieleza kuwa tayari miamba hiyo imeshafikia makubaliano ya ada ya mwanzo ya uhamisho ya pauni milioni18.1 na nyongeza(bonus) ya pauni milioni 4.2 endapo mchezaji huyo atafanya mambo makubwa zaidi.

Torres, ambaye amecheza EPL kwa takribani miaka 7 akiwa na Liverpoo na baadaye Chelsea, amesisitiza kuwa Pedro ana uwezo wa kucheza England hasa ikizingatiwa anataka nafasi zaidi ya kucheza.

“Ni rafiki yangu sana, na endapo ataamua kuelekea Uingereza, basi naamini atafanya vizuri tu”. Torres aliliambia Daily Mirror.


“Ana sifa zote za kukipiga EPL, amekuwa Barcelona kwa miaka mingi sana, hivyo naamini ana uwezo mkubwa ukiongezea pia na nidhamu ya uwajibikaji wake uwanjani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox