Timu za TP Mazembe ya Congo DRC na Mamelodi Sundowns ya nchini Afrika Kusini zinatarajiwa kuwasili Tanzania kwa ajili ya kucheza mashindano maalumu ya kumuaga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete anayemaliza muda muda wake madarakani kama Rais mwezi Octoba mwaka huu.
Klabu hizo zitaongozana na wamiliki wake ambapo Moise Katumbi ataongozana na klabu yake ya TP Mazembe kwenye safari hiyo ya kuja Tanzania wakati Patrice Motsepe nae atakuja pamoja na timu yakeya Mamelodi Sundowns kuja kumuaga Rais Kikwete katika mashindano hayo maalumu .
Kwa upande wa Tanzania, timu mbili zitakazothibitisha mapema ushiriki wake kati ya Azaim FC, Yanga SC na Simba SC zitapata fursa ya kushiriki mashindano hayo maalumu ya kumuaga Dkt. Jakaya Kikwete ambayo yatashirikisha timu nne mbili zikiwa ni TP Mazembe na Mamelodi Sundowns na timu mbili za Tanzania.
Rais Kikwete anafahamika kwa kuwa miongoni mwa marais wa Tanzania ambao wanapenda michezo na amesaidia kwa kiasi kikubwa kukua na kuendelea kwa michezo nchini husunan soka katika kipindi chote ambacho amekuwa madarakani.
Tarehe rasmi na ratiba ya mashindano hayo maalum bado haijapangwa
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni