Mtu
hatari: Mshambuliaji wa zamani wa Atletico Madrid, Costa akikimbia
baada ya kufunga bao lake la kwanza akiwa na jezi ya bluu ya Chelsea
MABAO
ya Diego Costa na Kurt Zouma yameipa Chelsea ushindi wa 2-1 dhidi ya
Olimpija Ljubljana jioni hii nchini Slovenia katika mchezo ambao Didier
Drgoba aliyerejeshwa tena Stamford Bridge alikuwa benchi
.
.
Kikosi
cha Jose Mourinho kililazimika kupambana na kutoka nyuma kwa bao 1-0
hadi mapunziko baada ya Nik Kapun kuifungia timu hiyo ya Slovenia bao la
kuongoza. Lakini mabao ya kipindi cha pili ya Costa na Zouma yaliipa
The Blues ushindi ikitoka nyuma.
Branislav
Ivanovic alifikiri amefunga bao la tatu, baada ya awali kukubaliwa,
lakini ghafla refa akabadilisha mawazo yake na kukataa bao hilo.
Kikois
cha Chelsea kilikuwa: Delac/Cech dk46, Azpilicueta/Ivanovic dk46,
Cahill/Terry dk46, Zouma, Luis/Ake dk46, Matic,Solanke, Fabregas/Romeu
dk69, Salah/Chalobah dk72, Boga/Van Ginkel dk46, Brown/Torres dk46 na
Costa/Bamford dk72.
Diego Costa akijiandaa kufunga
Costa akipambana na Antonio Mlinar Delamea
Orders: Manager Jose Mourinho shouts instructions from the half way line as his team take on Olimpija
Kurt Zouma (wa pili kushoto) akishangilia bao lake na Mohamed Salah
Kiungo wa zamani wa Arsenal na Barcelona, Fabregas alikuwa kivutioa leo
Mchezaji mpya, Filipe Luis (kulia) akipambana na Nik Omladic (kushoto)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni