STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 16 Machi 2016

AZAM WAIKAMATA TENA YANGA, KAPOMBE SHUJAA AFUNGA BAO PEKEE, ANGALIA MSIMAMO ULIVYO

Mabingwa wa klabu bingwa Afrika mashariki na kati Azam FC, wamefanikiwa kuvuna pointi tatu mbele ya Stand united katika muendelezo wa michezo ya ligi kuu ya Tanzania Bara.

Katika mchezo huo uliopaswa kuchezwa mwanzoni wa mwezi februari, ulishuhudia kipindi cha kwanza kumalizika bila kufungana, huku Azam FC wakitawala mchezo huo kwa kucheza pasi fupi fupi.


Azam FC walitengeneza nafasi tatu katika kipindi cha kwanza na kushindwa kuitumia huku Stand united wakitengenza nafasi moja ya wazi.

Kipindi cha pili kilirejea kwa kasi huku kila timu ikishambuliana kwa zamu na Azam FC kubadilisha aina ya uchezaji na kuanza kutumia mipira mirefu, wakati wa kupandisha mashambulizi.

Dakika ya 63 krosi ya mtokea benchi John Bocco, iliungwa vyama na Shomari Kapombe na kuindikia Azam FC goli la kuongoza.

Kuingia kwa goli hjilo kulipeleka Azam FC muda mwingi kuchezea mpira katika eneo lao, huku na marachache kutumia mipira mirefu kuwatafuta washambuliaji wao.

Stand united waliongeza kasi na kutengeneza nafasi mbili ambazo pia walishindwa kuzitumia na kupeleka mchezo kumalizika kwa Azam FC kuibuka na ushindi wa goli 1-0, na kupunguza wigo wa pointi baina yake na kinara Simba SC.


Kikosi cha Azam FC kilikuwa: Aishi Manula, Shomari, Kapombe, Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Serge Wawa, Jean Baptiste Mugiraneza, Frank Domayo, Mudathir Yahya/Kipre Balou dk79, Allan Wanga/John Bocco dk64, Kipre Tchetche na Farid Mussa/Waziri Salum dk65. 
 
Stand United: Frank Muwenge, Nassor Said ‘Chollo’, Suleiman Mrisho, Revocatus Richard, Assouman N'guessang, Jocob Masawe, Pastory Athanas, Amri Kiemba, Frank Hamis, Suleiman Kassim ‘Selembe’/Salum Kamana dk80 na Haruna Chanongo/Vitaris Mayanga dk68.



MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM

RnTimuPWDLFAGdPts
1SIMBA SC23173341132854
2YANGA21155151114050
3Azam FC21155137132450
4MTIBWA SUGAR21116426141239
5T. PRISONS239952120136
6MWADUI FC239772219334
7STAND UNITED2393111921-230
8NDANDA FC225981923-424
9MBEYA CITY2366112230-824
10MAJIMAJI FC2366111332-1924
11TOTO AFRICANS225891930-1123
12KAGERA SUGAR2357111725-822
13JKT RUVU2356122333-1021
14MGAMBO SHOOTING2348111828-1020
15AFRICAN SPORT235513926-1720
16Coastal Union2347121529-1419
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox