Katika mchezo huo uliopaswa kuchezwa mwanzoni wa mwezi februari, ulishuhudia kipindi cha kwanza kumalizika bila kufungana, huku Azam FC wakitawala mchezo huo kwa kucheza pasi fupi fupi.
Azam FC walitengeneza nafasi tatu katika kipindi cha kwanza na kushindwa kuitumia huku Stand united wakitengenza nafasi moja ya wazi.
Kipindi cha pili kilirejea kwa kasi huku kila timu ikishambuliana kwa zamu na Azam FC kubadilisha aina ya uchezaji na kuanza kutumia mipira mirefu, wakati wa kupandisha mashambulizi.
Dakika ya 63 krosi ya mtokea benchi John Bocco, iliungwa vyama na Shomari Kapombe na kuindikia Azam FC goli la kuongoza.
Kuingia kwa goli hjilo kulipeleka Azam FC muda mwingi kuchezea mpira katika eneo lao, huku na marachache kutumia mipira mirefu kuwatafuta washambuliaji wao.
Stand united waliongeza kasi na kutengeneza nafasi mbili ambazo pia walishindwa kuzitumia na kupeleka mchezo kumalizika kwa Azam FC kuibuka na ushindi wa goli 1-0, na kupunguza wigo wa pointi baina yake na kinara Simba SC.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa: Aishi Manula, Shomari, Kapombe, Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Serge Wawa, Jean Baptiste Mugiraneza, Frank Domayo, Mudathir Yahya/Kipre Balou dk79, Allan Wanga/John Bocco dk64, Kipre Tchetche na Farid Mussa/Waziri Salum dk65.
Stand United: Frank Muwenge, Nassor Said ‘Chollo’, Suleiman Mrisho, Revocatus Richard, Assouman N'guessang, Jocob Masawe, Pastory Athanas, Amri Kiemba, Frank Hamis, Suleiman Kassim ‘Selembe’/Salum Kamana dk80 na Haruna Chanongo/Vitaris Mayanga dk68.
MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM
Rn | Timu | P | W | D | L | F | A | Gd | Pts |
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
1 | SIMBA SC | 23 | 17 | 3 | 3 | 41 | 13 | 28 | 54 |
2 | YANGA | 21 | 15 | 5 | 1 | 51 | 11 | 40 | 50 |
3 | Azam FC | 21 | 15 | 5 | 1 | 37 | 13 | 24 | 50 |
4 | MTIBWA SUGAR | 21 | 11 | 6 | 4 | 26 | 14 | 12 | 39 |
5 | T. PRISONS | 23 | 9 | 9 | 5 | 21 | 20 | 1 | 36 |
6 | MWADUI FC | 23 | 9 | 7 | 7 | 22 | 19 | 3 | 34 |
7 | STAND UNITED | 23 | 9 | 3 | 11 | 19 | 21 | -2 | 30 |
8 | NDANDA FC | 22 | 5 | 9 | 8 | 19 | 23 | -4 | 24 |
9 | MBEYA CITY | 23 | 6 | 6 | 11 | 22 | 30 | -8 | 24 |
10 | MAJIMAJI FC | 23 | 6 | 6 | 11 | 13 | 32 | -19 | 24 |
11 | TOTO AFRICANS | 22 | 5 | 8 | 9 | 19 | 30 | -11 | 23 |
12 | KAGERA SUGAR | 23 | 5 | 7 | 11 | 17 | 25 | -8 | 22 |
13 | JKT RUVU | 23 | 5 | 6 | 12 | 23 | 33 | -10 | 21 |
14 | MGAMBO SHOOTING | 23 | 4 | 8 | 11 | 18 | 28 | -10 | 20 |
15 | AFRICAN SPORT | 23 | 5 | 5 | 13 | 9 | 26 | -17 | 20 |
16 | Coastal Union | 23 | 4 | 7 | 12 | 15 | 29 | -14 | 19 |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni