STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 21 Machi 2016

YANGA WAANZA MIKAKATI DHIDI YA AL AHLY YA MISRI..........

 

KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm kesho anatarajiwa kuwasilisha programu yake ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Al Ahly ya Misri katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

 

Yanga itamenyana na wababe wao wa kihistoria katika michuano ya Afrika, Al Ahly ya Misri katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Aprili 9, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kabla ya timu hizo kurudiana Aprili 19, Cairo, Misri.
 
 
Na baada ya Ahly kuinyanyasa kwa miaka mingi Yanga kwenye michuano yote ya CAF, safari hii wana Jangwani wamepania kuvunja mwiko kwa kuhakikisha wanawang’oa Waarabu hao.
 
Na kesho, Kamati ya Mashindano chini ya Mwenyekiri wake, Isaac Chanji itakutana na benchi la Ufundi chini ya kocha Pluijm na Msaidizi wake, Juma Mwambusi kujadili programu ya maandalizi.

 Tokeo la picha la Hans van der Pluijm  
Lakini tayari programu hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ratiba za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup – maana yake Yanga haiwezi kwenda kuweka kambi nje ya mji.
  Dhamira ya Yanga ilikuwa ni kwenda kuweka kambi Pemba, lakini Machi 31 wana mechi ya Kombe la TFF na Aprili 2 wana mechi ya Ligi Kuu, hivyo watalazimika kubaki Dar es Salaam.
  Na Dar es Salaam japokuwa wanaweza kupata hoteli nzuri ya kuweka kambi, lakini tatizo ni Uwanja mzuri wa mazoezi, kutokana na kukataliwa kufanya mazoezi Uwanja wa Taifa.
  Ahly imefuzu hatua hii baada ya kuitoa Recreativo do Libolo ya Angola kwa ushindi wa jumla wa 2-1, iliyoupata Cairo baada ya sare 0-0 Angola, wakati Yanga imeitoa APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2 ikishinda 2-1 Kigali na kulazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
  Mara ya mwisho timu hizo zilikutana mwaka 2014 katika Raundi ya Kwanza na Yanga ikatolewa kwa penalti 4-3, baada ya sare ya jumla ya 1-1, kila timu ikishinda 1-0 nyumbani kwake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox