STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 7 Aprili 2016

DUUUH: TANZANIA YAPOROMOKA NAFASI TANO KWENYE VIWANGO VYA FIFA


Tanzania

Kenya imeshuka hatua 12 nayo Tanzania ikashuka hatua 5 kwenye orodha ya viwango vya ubora wa soka ya Fifa iliyotolewa leo.

Kenya kwa sasa wamo nambari 115 nao Tanzania nambari 130.

Harambee Stars wameshuka baada ya kushindwa mechi mbili za kufuzu kwa Kombe la Mataifa Bingwa Afrika na Guinea Bissau.

Taifa hilo la Afrika Magharibi limepanda hatua 45 hadi nambari 102.
Guinea Bissau waliichapa Kenya 1-0 mechi ya kwanza tarehe 23 Machi na kwenye mechi ya marudiano wakashinda tena 1-0 jijini Nairobi.
Tanzania hawajahesabiwa mechi yoyote ya karibuni. Walishinda 1-0 dhidi ya Chad mechi ya kwanza ugenini lakini Chad wakajiondoa na hawakushiriki mechi ya marudiano jijini Dar es Salaam. CAF ilifuta matokeo hayo dhidi ya Chad katika kundi G.

Miongoni mwa mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nambari 72, Rwanda inafuata nambari 87, Kenya nambari 115, Burundi nambari 122, Tanzania nambari 130 na Sudan Kusini nambari 155.

Orodha ya mataifa kumi bora Afrika ni kama ifuatavyo:
  1. Algeria
  2. Ivory Coast
  3. Ghana
  4. Senegal
  5. Misri
  6. Cape Verde
  7. Tunisia
  8. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
  9. Guinea
  10. Congo
Duniani, orodha ya kumi bora ni kama ifuatavyo:
  1. Argentina
  2. Ubelgiji
  3. Chile
  4. Colombia
  5. Ujerumani
  6. Uhispania
  7. Brazil
  8. Ureno
  9. Uruguay
  10. England

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox