STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 18 Agosti 2016

SAMATA AFANYA YAKE GENK IKITANGULIZA MGUU MMOJA KUIFUATA MAN UNITED EUROPA

Katika raundi ya 4 ya mchujo wa kucheza hatua ya makundi ya michuano ya Europa League , Klabu ya KRC Genk anayokipiga mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania , Mbwana Samatta imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuza hatua ya makundi baada ya kutoka sare ya goli 2 – 2 na NK Lokomotiva ya Croatia .
Genk inanafasi nzuri ya kufuzu kutokana na kuwa na goli 2 za ugenini pale timu hizo zitakaporudiana wiki ijayo . Genk walianza kupata bao dakika ya 37   baada ya mchezaji wa Lokomotiva kuunawa mkono ndani ya box na kumfanya Leon Bailey afunge goli la kwanza la Genk .
Hadi Mpira unakwenda mapumziko , Genk ilikua inaongoza kwa bao 1 – 0 , ambapo dakika 2 baadae , Mtanzania Mbwana Samatta aliweza kuongeza bao la pili , baada ya kupokea krosi nzuri kutoka kwa Sandy Walsh na kuwafanya Genk waamini safari ya makundi kuwa imetimia .
Mbwana-Samatta-Genk-Europa-League-Bongosoka
Timu changa ya Lokomotiva haikutaka kukata tamaa mapema na kuendelea kupigana ambapo dakika ya 52 MirkoMaric aliifungia bao la 1 na dakika 7 baadae Ivan Fiolic aliweza kusawazisha kwa kufunga bao la pili .
Mbwana-Samatta-Genk-Europa-League-Bongosoka-2
Wiki ijayo , Tarehe 25 Agosti timu hizi mbili zitarudiana nyumbani kwa KRC Genk ambapo mechi hii ndio itaamua rasmi timu gani itasonga mbele kwenye hatua ya makundi 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox