TEVEZ AKIWA NA SEGUNDO SIKU CHACHE HUKO NYUMA... |
Baba wa mshambuliaji wa Juventus, Carlos Tevez aliyekuwa ametekwa amechiwa baada ya watekaji kulipwa kiasi kikubwa cha fedha.
Ingawa imekuwa ni siri
kiasi gani wamelipwa, lakini magazeti ya Argentina na vyombo vingine vya habari
vimeeleza, familia ya Tevez imelazimika kutoa mamilioni ya fedha kumuokoa
Segundo Tevez.
Baba huyo alitekwa baada
ya gari alilokuwa akisafiria kuzuiwa na watekaji hao katika eneo la Morón,
Magharibi mwa jiji la Buenos Aires.
Mwanasheria wa familia ya
Tevez, Gustavo Galass, amesema Segundo Tévez alitekwa na wahusika wakapiga simu
kwenye familia hiyo na kudai fedha huku wakitoa saa nane tu kabla ya kuchukua
uhai wake
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni