BABA
wa mchezaji wa zamani wa Manchester United na Manchester City, Carlos
Tevez ametekwa nchini Argentina, kwa mujibu wa taarifa.
La
Nacion ya Argentina imeripoti kwamba Juan Carlos Cabrera alikuwa
anaendesha gari lake katika Manispaa ya Moron, jimbo la Buenos Aires,
wakati anatekwa asubuhi ya leo.
Klabu
ya Tevez, Juventus imethibitisha kwamba mshambuliaji huyo amekwenda
Argentina baada ya tukio hilo asubuhi ya leo. Pamoja na hayo, klabu
haina taarifa zaidi juu ya tukio hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni