Sasa ni mwekundu wa Anfield: Lovren akiwa ameshika jezi ya Liverpool viwanja vya mazoezi vya timu hiyo, Melwood
BEKI wa kimataifa wa Croatia, Dejan Lovren amekamilisha uhamisho wake kutua Liverpool kwa dau la Pauni 20 kutoka Southampton.
Sasa
mchezaji huyo anaweka rekodi ya kuwa beki ghali zaidi kuwahi kusajiliwa
na Wekundu hao wa Anfield akipiku dau la Pauni Milioni 18.6, ambalo
Liverpool ililipa kumsajili beki wa Paris St Germain, Mamadou Sakho
Septemba mwaka jana.
Lovren,
ambaye amekuwa mlengwa chaguo la kwanza la beki wa kati katika mawindo
ya kocha Brendan Rodgers dirisha hili la usajili, amesaini mkataba wa
miaka minne baada ya kufuzu vipimo vya afya Merseyside.
Watano walionunuliwa kabla:
-Straika: Rickie Lambert, Miaka 32, Pauni Milioni 4 kutoka Southampton
-Kiungo: Adam Lallana, Miaka 25, Pauni Milioni 25 kutoka Southampton
-Kiungo: Emre Can, Miaka 20, Pauni Milioni10 kutoka Bayer Leverkusen
-Winga: Lazar Markovic, Miaka 20, Pauni Milioni 20 kutoka Benfica
-Beki: Dejan Lovren, Miaka 25, Pauni Milioni 20 kutoka Southampton
-Straika: Rickie Lambert, Miaka 32, Pauni Milioni 4 kutoka Southampton
-Kiungo: Adam Lallana, Miaka 25, Pauni Milioni 25 kutoka Southampton
-Kiungo: Emre Can, Miaka 20, Pauni Milioni10 kutoka Bayer Leverkusen
-Winga: Lazar Markovic, Miaka 20, Pauni Milioni 20 kutoka Benfica
-Beki: Dejan Lovren, Miaka 25, Pauni Milioni 20 kutoka Southampton
Dejan Loven ametua kwa dau la Pauni Milioni 20 kutoka Southampton
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni