STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 27 Julai 2014

LOGARUSIC AICHAMBUA SIMBA B NA KUSEMA; “MCHEZAJI MMOJA TU PALE”


Loga katikati akiwa na Kocha Msaidizi, Suleiman Matola kulia na Mwenyekiti wa Kamati ya Vijana, Said Tuliy kushoto 

KOCHA Mkuu wa Simba SC, Mcroatia Zdravko Logarusic amesema kwamba katika timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya klabu hiyo, ameona mchezaji mmoja tu anayefaaa kwa kikosi chake cha kwanza.
Logarusic aliyasema hayo jana Uwanja wa Karume, Dar es Salaam baada ya Simba B kutolewa na Azam FC katika Robo Fainali ya michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 20 kwa nchi za Maziwa Makuu, Rollingston kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90.
“Nimeona mchezaji mmoja tu,”alisema Logarusic alipoulizwa kuhusu Simba B, ameona vipaji vingapi kwa ajili ya kikosi cha kwanza baadaye.
“Simba ni timu kubwa, lazima mchezaji aonyeshe uwezo sana kudhihirisha yuko tayari kucheza timu kubwa kama hii,”aliongeza.
Hata hivyo, Logarusic hakuwa tayari kumtaja mchezaji aliyemvutia kutoka kikosi hicho kwa kuhofia kuwakatisha tamaa wengine. “Wanatakiwa wajibidiishe sana kufikia kiwango cha kuchezea Simba SC, kwa sasa bado sana,”aliongeza. 
Lakini katika kikosi cha Simba B kilichoishia Robo Fainali ya michuano ya Rollingston, kuna wachezaji watatu waliosajiliwa kwa ajili ya timu ya wakubwa- ambao ni Peter Manyika, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na Ibrahim Hajibu.   
Maneno ya Loga ni ujumbe wa wazi kwao- kwamba wanakabiliwa na changamoto ya kupandisha uwezo wao kama wanataka kupata nafasi katika kikosi cha kwanza cha Wekundu hao wa Msimbazi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox