STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 5 Agosti 2014

BOBBY WILLIAMSON KOCHA MPYA STARS


Mzoefu Afrika Mashariki; Bobby Williamson alifanya vizuri akiwa na Uganda na sasa anahamishia mafanikio hayo Kenya 

KOCHA wa Gor Mahia, Bobby Williamson amateuliwa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars na anatakiwa kuanza kazi mara moja.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF), Sam Nyamweya amethibitisha uteuzi wa kocha huyo wa zamani wa Uganda, Cranes katika Mkutano na Waandishi wa Habari leo Nairobi Hotel. 
Wanasoka wa zamani wa kimataifa wa Kenya, Mussa Otieno na Simon Mulama pia wameteuliwa kuwa Wasaidizi wa kocha huyo na Meneja.
Jukumu la kwanza la Mscotland huyo litakuwa ni kutetea Kombe la Mataifa ya Afrika Mashaiki na Kati, CECAFA Challenge Novemba mwaka huu.
Kocha huyo aliingia Afrika Mashariki Agosti mwaka 2008 alipopewa jukumu la kuifundisha Uganda Cranes ambako alidumu kwa miaka mitano kabla ya kuhamia Gor Mahia Julai 5 mwaka 2013.
Bobby anachukua nafasi ya Adel Amrouche aliyefukuzwa baada ya Kenya kushindwa kuingia kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Morocco, kwa kutolewa na timu dhaifu, Lesotho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox