STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 21 Agosti 2014

ORODHA YA MAJERUHI YAANZA ASERNAL, MIKEL ARTETA NJE MECHI MBILI

Sidelined: Arsenal midfielder Mikel Arteta has been ruled out of the Gunners next two fixtures
Majanga: Kiungo wa Arsenal, Mikel Arteta atakaa nje ya uwanja kwa mechi mbili zijazo.

HABARI mbaya kwa mashabiki wa Asernal, Mikel Arteta atakaa nje ya uwanja katika mechi mbili zijazo baada ya kupata majeruhi ya kifundo cha mguu wakati wa mechi ya mtoano ligi ya mabingwa barani Ulaya jumanne ya wiki hii dhidi ya Besiktas.
Nahodha huyo wa Asernal alitolewa katika dakika ya 50 ndani ya dimba la Olympic Ataturk Stadium kufuatia kugongana na mshambuliaji wa zamani wa Cheslea, Demba Ba.
Pia Asernal itamkosa Aaron Ramsey katika mchezo wa marudiano dhidi ya timu hiyo ya Uturuki baada ya kuoneshwa kadi nyekundu katika mchezo wa kwanza ugenini.
Painful: Arteta sprained his ankle against Besiktas and will miss Saturday's clash against former club Everton
Maumivu: Arteta aliumia kifundo cha mguu.

Arteta atakosa mechi ya jumamosi ya ligi kuu ugenini dhidi ya Everton na mechi ya marudiano ya ligi ya mabingwa katika uwanja wa Emirates dhidi ya Besiktas jumanne ijayo.
Nyota huyo atapimwa zaidi leo alhamisi, lakini ni wazi kuwa atakosa mechi mbili zijazo.
Orodha ya majeruhi kwa Asernal tayari imeanza ambapo Yaya Sanogo na Kieran Gibbs walikosa mechi ya suluhu ya bila kufungana mjini Istanbul.

HISTORIA INAWABEBA VIJANA WA ASERNE WENGER

Haitakuwa kazi rahisi kwa Arsenal  kushinda mechi ya marudiano hususani ikiwakosa Aaron Ramsey na Mikel Arteta, lakini hawajawahi kutolewa hatua ya kufuzu ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.

2013-14 - Waliifunga Fenerbahce kwa wastani wa mabao 5-0 , walifika raundi ya pili.

2011-12 - Waliifunga Udinese kwa wastani wa mabao 3-1 , walifika raundi ya pili.

2009-10 - Waliitoa Celtic kwa wastani wa mabao 5-1, walifika robo fainali

2008-09 - Waliitoa  FC Twente kwa wastani wa mabao 6-0 , walifika nusu fainali.

2007-08 - Waliifunga Sparta Prague kwa wastani wa mabao 5-0, walifika robo fainali

2006-07 - Waliitoa Dynamo Zagreb kwa wastani wa mabao  5-1, walifika raundi ya pili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox