STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 21 Agosti 2014

SOMA MASHAIRI YA WIMBO MPYA WA FID Q AKIMSHIRIKISHA P. FUNK - BONGO HIPHOP..



VERSE 1:

Ulianza wewe.. wakaja waimbaji na wabana pua/
Wale mwewe.. Franga wawindaji wakatusua/
Kwakuwa.. wanajua mshikaji unaishi kwa miko/na zako itikadi.. ziko kimziki na sio mshiko/
Kama haileti hela..basi haimake sense.. no sweat kisela mie nikakomaa tu na lako penzi/
Sikusound garbage au kuchange suddenly../
Mie ni mjeshi so naweza fight savagely/
Hiphop ya ukweli.. ukapigwa radioni/sometimes malaika wa heri nao hutembelea motoni/
Penzi ni kipofu na anayemuona halioni/ sikuwa na hofu.. mama alinipenda tangu nikiwa tumboni/
I started young.. I made my mother's womb a drum/
My umblirical chord a guitar.. muhoji aliyenizaa/
BONGOFLAVA mzuri kiasi.. hiphop we ndo my queen/ my 1st.. my last & everything in betweenjj



Chorus:

Mimi na wewe.. tangu long time/ Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame/
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2
'

VERSE 2:

Kama kukupenda wewe ni dhambi.. basi shetani yu nami/ na kamwe sintonyea kambi ili niwabambe dukani/
For a million little pieces naweza kumcon Oprah ka James Frey/
Na watasema sitishi wakati wanaogopa nisitokee/
Waufuate mkumbo huu wa wasomi.. wa midundo na mistari/ ukiwa na nyundo mkononi.. ni rahisi kupigilia msumari/
Sio tu bongo.. mpaka Ng'ambo hakuna uhuru wa habari/ kuna uhuru wa mwenye chombo.. mitambo na mwenye mali/
Kujifanya hawasikii.. haiwasaidii.. wala haiwajengi/ unachosema ni.. kamwe IPP haitompinga Mengi/
Unawakumbusha wazazi wa uswazi.. chati ya uteja imeingia/ na Mapusha wanauza drugs ili walishe familia/
Mbaya.. kuhifadhi fuvu la mtu ndani ya kabati/ mbaya zaidi ni kuwa na ndugu.. halafu kichwa maji/
Amka bongo lala.. hiphop sio ufala.. ni lazima uifate/
Uaminifu ni kama mshahara.. fanya kazi ili uupate

Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time/ Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2




VERSE 3:
Mapenzi ya sikuhizi.. bila kugombana yanakua hayana stimu/
Pia ni ruksa kushikana lakini sio kushikiana simu/
Inanipa wazimu.. kusikia kimwana haujaachana na Hasheem/
Na bado mnawasiliana..una mpango wa kuchanganya timu?/
Nakupenda hiphop.. ndo maana ninarap ile mbaya/
Naspit fire bila hennessy.. au kula kaya/
I want my art to be my legacy.. kabla sijaretire.. waanze nigwaya hawa enemies.. anyways NI HAYO TU/
Beef huletwa na wivu.. na wivu sio hiphop/




Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time/ Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame/
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox