STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 5 Agosti 2014

TAKWIMU ZA KUFUNGA NA KUFUNGWA MAGOLI KATI YA YANGA NA AZAM FC, MSIMU UJAO NANI ATATISHA?


AZAM FC waliibuka mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita kwa kuwashinda waliokuwa washindani wao wakubwa, Yanga sc na Mbeya  City fc kwa mbali.
Hizi ni rekodi za mabao msimu wa 2013/2014 ambao ulikuwa na ushindani mkubwa hususani katika mbio za ubingwa.
Azam fc ndio timu iliyofungwa mabao machache zaidi kuliko timu zote 14 za ligi kuu ambapo iliruhusu nyavu zake kuguswa mara 15 tu.
Yanga sc ndio timu iliyofunga mabao mengi zaidi msimu uliopita ambao ilitikisha nyavu za wapinzani mara 61.
Azam ilikuwa timu ya pili kufunga mabao mengi ambapo ilitia kambani magoli 51.
Licha ya Yanga kufunga mabao mengi, lakini ilifungwa magoli mengi ukilinganisha na mabingwa Azam ambapo iliruhusu nyavu zake kuguswa mara 19 .
Mbeya City na Kagera Sugar zilikuwa timu zinazofuatia kufungwa mabao machache zaidi ambapo kila moja iliruhusu nyavu zake kuguswa mara 20.
JKT Ruvu ndio timu iliyofungwa mabao mengi zaidi msimu uliopita ambapo nyavu zake ziliguswa mara 40, ikifuatiwa na timu za Rhino Rangers na Ashanti United zilizofungwa mabao 39.
Rhino na Ashanti zilishashuka daraja na kuzipisha Stand United ya Shinyanga, Ndanda fc ya Mtwara na Polisi Morogoro ya mkoani Morogoro.
Kwa kuangalia takwimu hizi za mabao unaweza kusema:
Azam fc ndio timu iliyokuwa na safu bora zaidi ya Ulinzi ikifuatiwa na Dar Young Africans.
Aggrey Morris, Said Mourad Mwenda, David Mwantika, Erasto Nyoni, Gadile Michael na wengineo, walifanya kazi nzuri zaidi ya mabeki wa timu zote 14 za ligi kuu.
Kwa upande wa Yanga, Nadir Haroub `Canavaro’, Kevin Yondan, Oscar Joshua, Mbuyu Twite na wengineo walijitahidi kufuata nyayo za mabeki wa Azam fc.
Mbeya City na Kagera zilishika nafasi ya tatu kuwa na safu imara ya ulinzi kwa maana ya kuruhusu magoli machache.
Yanga ndio timu iliyokuwa na safu kali zaidi ya ushambuliaji ikifuatiwa na Azam fc, lakini moja ya mshambuliaji wake, Didier Kavumbagu ameshaondoka.
Lakini wamewasajili Wambrazil wawili, kiungo mshambuliaji, Andrey Coutinho na mshambuliaji Gleison Santos Santana ‘Jaja’. Pengi wataziba pengo hilo, ingawa wanatakiwa kumuacha mchezaji mmoja wa kigeni baada ya kuzidisha idadi.
Niyonzima, Twite, Kiiza na Okwi, lazima mmoja nyumba imuangukie. Lakini inaonakana vita ni kati Okwi na Kiiza, lazima mmoja aondoke.
JKT Ruvu ndio timu iliyokuwa na safu mbovu zaidi ya ulinzi kuliko timu zote 14. Kwa maana hiyo, safu ya ulinzi lazima iimarishwe wakati huu wa usajili pamoja na kutafuta viungo watakaotoa msaada kwa mabeki.
Kwa kuzingatia takwimu hizi za mabao, inategemewa kuona Azam fc inaongeza nguvu safu ya kiungo na ushambuliaji. Kwa maana ya kupata viungo watakaochezesha safu yao ya ushambuliaji.
Yanga wanatakiwa kuimarisha kiungo na ulinzi. Inaonekana licha ya kuwa na washambuliaji wakali, lakini sehemu ya kiungo iliyumba na kuwapa kazi mabeki kuzuia hatari na matokeo yake kushika nafasi ya pili kwa kufungwa mabao machache.
Lakini takwimu sio mbaya sana, Yanga ilikuwa timu ya pili iliyoonekana kuwa imara idara zote, japokuwa kulikuwa na mapungufu katikati na beki.

Je, wachezaji wanosajiliwa Yanga na Azam ni wa aina gani?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox