STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 13 Septemba 2014

ARSENAL v MANCHESTER CITY: JACK WILSHERE, ALEXIS SANCHEZ WATATAMBA MBELE YA YAYA TOURE, SERGIO AGUERO EMIRATES?


ARSENAL wanaikaribisha Manchester City katika mechi ya ligi kuu England itakayopigwa Emirates mapema majira ya saa 8:45 mchana.
Msimu uliopita, Arsenal walitandikwa mabao 6-3 na kikosi cha Manuel Pellegrini katika uwanja wa Etihad, na leo hii wanaingia uwanjani wakitaka kulipa kisasi.
Itakuwa ni vita kali Emirates, nani ataibuka mbabe? dakika tisini zitaamua.
Mechi nyingine itawakutanisha Chelsea dhidi Swansea katika dimba la Darajani.
Crystal Palace watakuwa nyumbani kuchuana na Burnley, wakati Southampton nao watakuwa nyumbani dhidi ya Newcastle.
Stoke City watakuwa wenyeji wa Leicester na Sunderland watakuwa dimba la nyumbani kuchuana na Tottenham.
Nao West Brom watakuwa uwanja wa nyumbani kukabliana na Everton.
Majogoo wa jiji, Liverpool watakuwa nyumbani Anfield kuoneshana kazi na Aston Villa.
Ligi hiyo itandelea kesho ambapo Manchester United watakuwa na kibarua kizito Old Trafford kuchuana na QPR.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox