LIGI kuu nchini
Uingereza inaendelea tena leo ambapo kutakuwa na mchezo mmoja
utakaozikutanisha timu za Hull City na West Ham United katika Uwanja wa
Kingston Communication-KC.
Hull wataingia katika mchezo huo bila ya kuwa
na mshambuliaji wao tegemeo Abel Mathias Hernandez Platero. Nyota huyo
wa kimataifa wa Uruguay mwenye umri wa miaka 24 alisajiliwa na Hull
katika siku ya mwisho ya usajili akitokea klabu ya Palermo lakini
mashabiki watalazimika kusubiri kutokana na mchezaji huyo kuchelewa
kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza. Hata hivyo kocha wa Hull Steve
Bruce atapata ahueni baada ya kuwepo mshambuliaji mwingine wa kimataifa
wa Uruguay Gaston Ezequiel Ramirez Pereyra.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni