MENEJA wa klabu ya
Manchester United, Louis van Gaal ameanza kutamba kuwa anataka
kulirejesha taji la Ligi Kuu Old Trafford. Kauli ya kocha huyo Mholanzi
imekuja kufuatia ushindi mnono wa mabao 4-0 waliopata dhidi ya Queens
Park Rangers jana ukiwa ni ushindi wake wa kwanza toka achukue mikoba ya
kuinoa klabu hiyo katika kipindi cha majira ya kiangazi. Akihojiwa mara
baada ya mchwezo huo, Van Gaal amesema anataka kushinda taji la Ligi
Kuu kama sio msimu huu basi msimu unakuja au unaofuata lakini anataka
kuwapa furaha mashabiki wa klabu hiyo. Van Gaal ambaye amewahi kushinda
mataji ya ligi katika msimu wake wa kwanza wakati akizinoa Barcelona na
Bayern Munich, amewekewa malengo ya kumaliza katika nafasi tatu za juu
msimuu na Ofisa Mkuu Ed Woodward. Baada ya kufunga mabao mawili katika
mechi nne zilizopita chini ya Van Gaal, United jana walionyesha mchezo
mzuri dhidi ya QPR ambapo mabao yake yalifungwa na Angel Di Maria, Ander
Herrera, Wayne Rooney na Juan Mata.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatatu, 15 Septemba 2014
VAN GAAL AANZA KUCHONGA UNITED.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni