STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 28 Septemba 2014

SIRI YA POLISI MORO KUINYAMAZISHA SIMBA SC HII HAPA...

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
NAHODHA wa Polisi Morogoro Nicholas Kabipe amefichua siri ya kupata sare ya 1-1 dhidi ya Simba katika mchezo wa raundi ya pili ya ligi kuu soka Tanzania bara iliopigwa jana uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Simba walikuwa kwa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 32 kipindi cha kwanza kupitia kwa Emmanuel Okwi, lakini Danny David Mrwanda aliisawazishia Polisi katika dakika ya 50 kipindi cha pili.
Kabla ya mechi ya jana, Polisi walifungwa 3-1 na Azam fc katika mechi ya ufunguzi iliyochezwa wikiendi ya septamba 20 mwaka huu uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Baada ya mechi ya jana dhidi ya Simba, Kabipe alisema: “Kwa matokeo haya sisi tumefurahi kwasababu tulipoteza mchezo wa kwanza. Kuna makosa yalikuwa yanatugharimu na Azam wakatufunga magoli matatu.
“Tumerekebisha hayo makosa na tumeweza kupata sare. Wakati wa mapumziko tukiwa nyuma kwa goli moja kwa bila, mwalimu alituelekeza kuwa Simba wana kasi sana sehemu ya kiungo”.

“Kwahiyo akasema tunatakiwa tuwe wengi katikati ili tusiwape nafasi ya kucheza, tuwe tunaenda kukaba watu watatu na tulifanya hivyo, ikawezekana na tukaweza kupata sare hiyo”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox