STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 30 Septemba 2014

WACHEZAJI BAYERN WATOLEWA MBIO HOTELINI BAADA YA HOTEL WALIYOFIKIA KUWAKA MOTO


Wachezaji wa Bayern Munich, walilazimika kukimbia mbio wakitolewa kwenye hoteli mjini Moscow baada ya kuwa na taarifa ya moto.

Wachezaji hao wakiwa na kocha wao Pep Guardiola walilazimika kutimua mbio hadi nje ya hoteli baada ya kuwa na taarifa kwamba kuna moto kwenye moja ya sehemu ya hoteli hiyo.

Kikosi hicho kipo mjini humo kuivaa CSKA Moscow katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Wachezaji hao walikutana na wakati mgumu baada ya kutolewa nje ya hoteli kutokana na baridi kali mjini humo.

Hali hiyo iliwalazimu baadhi yao kuchukua mataulo ya hoteli na kujifunika ili kupambana na hali hiyo ya baridi kali.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox