KLABU ya AC Milan
imekanusha taarifa kuwa kiungo wa kimataifa wa Ghana Michael Essien
ameambukizwa ugonjwa wa Ebola wakati akiwa katika majukumu ya
kimataifa. Taarifa zilizozagaa nchini Ghana mwishoni mwa wiki iliyopita
zimedai kuwa Essien alikuwa akipatiwa matibabu baada ya kuambukizwa
virusi hivyo hatari. Hata hivyo klabu hiyo ya Serie A ilitoa taarifa
kukanusha taarifa hizo na kudai kuwa hazina ukweli wowote na hazijawahi
kuthibitishwa na mwajiriwa wao yeyote. Magazeti ya Daily Times na
Newswire yote ya Nigeria yalitoa taarifa iliyothibitishwa na AC Milan
ambayo inadai kuwa Essien aliambukizwa Ebola. Naye Essien mwenyewe
alituma picha katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa instagram na
kudai kuwa yuko fiti na mwenye afya tele na kukanusha tetesi zote
zinazomhusisha yeye kupata ugonjwa hatari. Essien aliongeza kuwa virusi
vya Ebola sio jambo la mzaha hivyo watu wanapaswa kutofanya utani na
suala hilo.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatatu, 13 Oktoba 2014
AC MILAN YAKANUSHA ESSIEN KUUGUA EBOLA.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni