LIGI Kuu ya Soka nchini
India ijulikanayo kama Indian Super League imeanza rasmi jana huku timu
ya Mumbai City ikichabangwa kwa mabao 3-0 na Atletico de
Kolkata. Nahodha wa zamani wa kriketi wa India Sachin Tendulkar, mmiliki
mwenza wa timu mojawapo katika ligi hiyo Kerala Blasters waliokuwa
miongoni mwa watu mashuhuri waliohudhuria ufunguzi wa ligi hiyo huko
Calcuatta. Wachezaji wa Mumbai Nicolas Anelka na Freddie Ljungberg
walikosa mchezo huo kutokana na majeruhi yanayowasumbua. Mabao katika
mchezo huo yalifungwa na Fikru Teferra, Borja Fernandez na Arnal Llibert
ambapo nyota wa zamani wa Liverpool Luis Garcia alikuwa akiichezea
Kolkata. Ligi hiyo inatarajiwa kudumu kwa muda wa wiki 10, ikishirikisha
timu nane kwa madhumuni ya kuibua umaarufu wa mchezo huo katika nchi
hiyo ambayo imetawaliwa kwa kiasi kikubwa na kriketi.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatatu, 13 Oktoba 2014
LIGI KUU INDIA YAZINDULIWA RASMI.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni