Amri Kiemba, Shabani Kisiga na Haruna
Chanongo wameamriwa kuondoka kwenye kambi ya na kurejea jijini Dar es Salaam.
Wachezaji hao watatu wanatuhumiwa kwa utovu
na taarifa zinaeleza kuwa asubuhi wataondoka kurejea Dar es Salaam kwa mabasi.
Uamuzi huo umefikiwa kwa pamoja na wajumbe
wa kamati ya utendaji ya Simba wanaowatuhumu kwa utovu wa nidhamu.
Baada ya hapo, wametakiwa kurejea Dar es Salaam
na Ijumaa ikiwa ni siku moja kabla ya Simba kuivaa Mtibwa Sugar mjini Mororogo,
wenye watawekwa kiti moto.
Wachezaji hao watawekwa kitimoto na kamati
ya utendaji ya Simba kuhojiwa kuhusiana na masuala ambayo yameelezwa ni ya
utovu wa nidhamu.
Viongozi wa Simba wamekuwa wagumu kulieleza
hilo, lakini taarifa zinasema iwapo kutabainika kuna tatizo, basi wachezaji hao
wataondolewa kabisa katika kikosi cha Simba.
Simba imetoka sare tano katika mechi zake
tano, nne ikiwa imecheza nyumbani hali inayosababisha presha kubwa Msimbazi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni