MSHAMBULIAJI
Edinson Cavani jana alikuwa miongoni mwa wachezaji watatu walioonyeshwa
kadi nyekundu wakati Paris St Germain ikiitandika RC Lens mabao 3-1
katika mchezo wa Ligue 1 Uwanja wa Stade de France.
Mwanasoka
huyo wa kimataifa wa Ufaransa alipewa kadi hiyo na refa Nicolas
Rainville, baada ya kushangilia bao la mwisho la timu yake kwa ishara ya
kupiga bunduki, staili maarufu kwa klabu ya Arsenal ya England.
Rais
wa PSG, Nasser Al-Khelaifi ameponda maamuzi hayo ya utata akisema
kwamba kama adhabu zitatolewa kwa ushangiliaji wa aina hiyo, ni mbaya
kwa soka ya Ufaransa. Mabao ya PSG yalifungwa na Cabaye dakika ya 28,
Maxwell dakika ya 33 na Cavani dakika ya 55, wakati Lens pia ilipoteza
wachezaji wawili waliotelewa kwa kadi nyekundu, Gbamin na Le Moigne,
huku bao lao la kufutia machozi likifungwa ma Coulibaly dakika ya 10.
Hiruhusiwi Ufaransa; Edinson Cavani akishangilia kwa staili ya mtutu wa bunduki kabla ya kutolewa kwa kadi nyekundu |
Mshambuliaji wa Paris Saint Germain, Edinson Cavani akiwa hamming macho yake wakati analimwa kadi nyekundu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni