Andres Iniesta amempiku
Cristiano Ronaldo na kutwaa tuzo ya unyayo wa dhahabu.
Tuzo hiyo imetolewa jana
jijini Monaco, Ufaransa na kawaida yake mtu hushinda tuzo hiyo mara moja tu.
Aliyekuwa anaishikilia
alikuwa ni Didier Drogba aliyeichukua mwaka jana akiwa Galatasaray ya Uturuki.
Pamoja na Ronaldo, Iniesta aliwapiku wachezaji
wengi walioingia fainali ambao ni Wayne Rooney, Manuel Neuer, Andrea Pirlo,Thiago Silva, Franck Ribery, Yaya Toure,Thierry Henry na
Marta.
Kawadia waandishi hufanya uchaguzi wa kupata wachezaji kumi wa
mwisho, baada ya hapo kura hupigwa kupitia mtandao kupata mshindi.
2003 - Roberto
Baggio, Brescia
2004 - Pavel Nedved, Juventus
2005 - Andriy Shevchenko, AC Milan
2006 - Ronaldo, Real Madrid
2007 - Alessandro Del Piero, Juventus
2008 - Roberto Carlos, Fenerbahce
2009 - Ronaldinho, AC Milan
2010 - Francesco Totti, Roma
2011 - Ryan Giggs, Manchester United
2012 - Zlatan Ibrahimovic, PSG
2013 - Didier Drogba, Galatasaray
2014 - Andres Iniesta, Barcelona
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni