MECHI za Kombe la Dunia
nchini Qatar zinaweza kumalizika usiku wa manane mpaka saa tisa alfajiri
kama mapendekezo yaliyotolewa na ofisa wa ngazi juu katika soka
yatafanyiwa kazi. Harold Mayne-Nicholls ambaye anatarajiwa kumpa
changamoto Sepp Blatter katika kinyang’anyiro cha urais wa Shirikisho la
Soka Duniani-FIFA mwakani, amesema michuano hiyo ya mwaka 2022 bado
inawezekana kufanyika katika majira ya kiangazi. Lakini Ofisa huyo wa
zamani wa soka wa Chile amesema baadhi ya michezo italazimika kuanza
usiku mkubwa ili kuepuka joto kali. Mayne-Nichollos aliendelea kudai
kuwa inawezekana mchezo wa kwanza ukachezwa saa moja za usiku, wa pili
saa nne na mchezo wa tatu ukaanza saa saba za usiku. Inategemewa
michuano hiyo ya Qatar kuhamishwa katika majira ya baridi ili kuepuka
joto kali huku FIFA wakifikiria kuipeleka Novemba na Desemba lakini
Mayne-Nicholls amesema kufanya hivyo kutavuruga ratiba ya ligi
mbalimbali duniani. Qatar walipewa uenyeji wa kuandaa michuano hiyo ya
mwaka 2022 na kamati ya utendaji ya FIFA mwaka 2010.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 21 Oktoba 2014
KIONGOZI ATOA WAZO LA MECHI ZA QATAR KUCHEZWA USIKU WA MANANE.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni