Kipa wa zamani wa kimataifa
wa Bosnia, ametoa kali baada ya kumtwanga mwamuzi konde kali.
Romeo Mitrovic, alimpiga
mwamuzi konde katika mechi ya daraja la pili, baada ya kulambwa kadi ya njano.
Kipa huyo aliyewahi
kuichezea timu yake ya taifa mwaka 2006 ilipochapwa mabao 2-0 dhidi ya Korea
Kusini, alionyesha kukerwa na kadi hiyo, hivyo kuchukua uamuzi huo mkali.
Alionyesha kadi baada ya
kupoteza muda, ilionekana kipa huyo wa HNK Branitelj kama alifanya mzaha.
Haraka akamkimbilia mwamuzi na kumchapa konde, mwamuzi akatimua mbio kuomba msaada wa askati ambao walimzunguka wakati akimpa kipa huyo kadi nyekundu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni