WINGA wa klabu ya
Arsenal, Lukas Podolski amedokeza kuwa anaweka kuikacha timu hiyo kabla
ya mkataba wake kumalizika mwaka 2016 kwasababu ya kukosa nafasi ya
kucheza mara kwa mara. Akihojiwa Podolski amesema ni mchezaji wa mtaani
ambaye damu inachemka hivyo anapenda kushindana na anakosa nafasi hiyo
kila mwishoni mwa wiki anapaswa kufanya mabadiliko. Podolski ambaye
ameifungiwa timu yake ya taifa ya Ujerumani mabao 47 katika mechi 118
alizocheza alijiunga na Arsenal mwaka 2012. Hakuhusishwa katika mechi
nne za ufunguzi wa msimu kufuatia mafanikio waliyopata Ujerumani katika
Kombe la Dunia nchini Brazil na amekuwa akisugua benchi katika nane
zilizopita za Arsenal. Nyota huyo amesema kwasasa anaangalia hali
inavyokwenda na kama mambo yakiendelea kuwa hivyo ataona kama kuna
uwezekano wa kutafuta timu atakayopata nafasi ya kucheza.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 2 Oktoba 2014
PODOLSKI ACHOSHWA NA BENCHI ARSENAL.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni