KLABU ya Manchester
United inajipanga kutoa ofa ya kitita cha euro milioni 13 kwa ajili ya
kumnasa kiungo wa Real Madrid Sami Khedira katika dirisha dogo la
usajili Januari mwakani. United imemua kuhamishia nguvu zao kwa kiungo
huyo wa kimataifa wa Ujerumani baada ya kuhabalishwa kuwa kiungo wa AS
Roma Kevin Strooman aliyekuwa akiwindwa na Louis van Gaal hataweza
kuondoka katika kipindi hicho. Van Gaal ameruhusiwa kutumia tena fedha
katika usajili wa Januari ili kuendelea kuimarisha kikosi cha United
baada ya kusajiliwa kwa Angel Di Maria, Ander Herrera na Radamel Falcao
katika majira ya kiangazi. Inafahamika kuwa Khedira yuko tayari kuondoka
na kwenda katika timu inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
lakini United wao wameonyesha wako tayari kumlipa mshahara wa paundi
255,000 kwa wiki anaouhitaji ili atue Old Trafford. Katika kipindi cha
kiangazi Khedira aliwekwa sokoni kwa kitita cha euro milioni 26 na
kulikuwa na tetesi za Arsenal kumuhitaji lakini walishindwana kutokana
na kiasi kikubwa cha mshahara alichohitaji.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 2 Oktoba 2014
MAN UNITED KUMTENGEA KHEDIRA EURO MILIONI 13 JANUARI.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni