MENEJA wa klabu ya
Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha leo kuwa atamkosa kiungo wake
majeruhi Aaron Ramsey kwa muda wa wiki nne au zaidi. Nyota huyo wa
kimataifa wa Wales alipata majeruhi ya msuli wa nyuma ya paja wakati wa
mchezo wa Ligi Kuu uliokwisha kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Tottenham
Hotspurs Jumamosi iliyopita hatua mbayo ilimfanya kukosa mchezo wa Ligi
ya Mabingwa Ulaya Jumatano. Vyombo vya habari nchini Uingereza
vimeripoti leo kuwa Ramsey anaweza kuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi
minne lakini Wenger amesema nadhani kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23
anaweza kurejea uwanjani mwanzoni mwa mwezi ujao. Wenger amesema kwa
mujibu wa madaktari Ramsey anaweza kuwa nje kwa muda wa wiki tatu mpaka
nne hivyo yeye ameamua kuhesabu nne kabisa. Kama nyota huyo akikaa nje
kwa muda huo ataikosa michezo ya Ligi Kuu dhidi ya Chelsea, hull City na
Sunderland pamoja na mchezo wa ugenini wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi
ya Anderlecht.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 3 Oktoba 2014
RAMSEY "PANCHA" TENA WENGER ATHIBITISHA KUWA NJE WIKI NNE.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni