KOCHA wa timu ya taifa
ya Hispania, Vicente Del Bosque amemuita Diego Costa katika kikosi chake
kwa ajili ya michezo ya kufuzu michuano ya Ulaya mwakani dhidi ya
Slovakia na Luxembourg, pamoja na Jose Mourinho kuonya kuwa mshambuliaji
huyo wa Chelsea anapaswa kutumiwa kwa uangalifu. Nyota huyo mwenye umri
wa miaka 25 amekuwa akisumbuliwa na majeruhi ya misuli hivi karibuni
huku Mourinho akidai kuwa Costa ni kama hafanyi kabisa mazoezi ili
kumuweza apone vizuri na kuelekeza kuwa ingefaa asiitwe kwa ajili ya
mechi za kimataifa. Hata hivyo Mourinho alimchezesha Costa kwa dakika
zote 90 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya walioshinda dhidi ya
Sporting Lisbon ikiwa ni mara ya kwanza kwa mshambuliaji huyo kucheza
muda wote baada ya kupita mwezi. Del Bosque ameuamua kujibu mapigo kwa
kumuita nyota huyo na kudai kuwa haoni tatizo lolote kwnai anacheza
mechi zote za klabu yake.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 3 Oktoba 2014
DEL BOSQUE AMUONYESHA JEURI MOURINHO KWA KUMUITA COSTA HISPANIA.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni