KLABU ya Arsenal ina
hamu kubwa ya kulipa kisasi kufuatia kipigo kikali walichopata kutoka
kwa Chelsea machi mwaka jana, aibu ambayo meneja Arsene Wenger amekiri
kuwa yeye pamoja na klabu hataweza kuisahau kamwe. Wenger atakuwa
akitafuta ushindi wa kwanza kwa kocha wa Chelsea Jose Mourinho kitu
ambacho hajawahi kupata katika michezo mingi ya Ligi Kuu ambayo
wamekutana chini ya kocha huyo Mreno. Hata hivyo Wenger anakiri kipigo
cha mabao 6-0 walichopata kutoka kwa Chelsea katika Uwanja wa Stamford
Bridge bado umewaachia jehara kubwa ambalo litakuwa vigumu kupona kwa
haraka. Wenger amesema hawataweza kusahau kilichowatokea mwaka jana na
sasa wana nafasi ya kuweka mambo sawa katika mchezo wa Jumapili. Wakiwa
wametofautiana kwa alama sita na Chelsea ambao ndio vinara wa ligi hiyo,
Wenger amesema ushindi ni muhimu katika mchezo huo kama wanataka
kubakia katika mbio za kufukuzia taji la ligi.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 3 Oktoba 2014
WENGER AKUMBUKA KICHAPO CHA 6-0 KUTOKA KWA MOURINHO.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni