RAIS wa klabu ya
Sporting Lisbon, Bruno de Carvalho amedai kuwa walikuwa chini ya
shinikizo kutoka nje ili wamuuze Marcos Rojo kwenda Manchester
United. De Carvalho amesema wamiliki wa tatu alihudhuria mikutano yao na
kuwafanya waamini kuwa ni maofisa wa United. Rais huyo alidai kuwa
walikuwa hawana mpango wa kumuuza Rojo kwakuwa alikuwa mchezaji muhimu
kwao. Beki huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 24 ambaye
alijiunga na Sporting Lisbon mwaka 2012 alisajiliwa na United kwa
kitita cha paundi milioni 16. De Carvalho amesema shinikizo lilikuwa
kubwa sana kwani watu walianza kuongeza na klabu na kwenda huko kwa
ajili ya mikutano. Umiliki wa tatu wa mchezaji umefungiwa nchini
Uingereza hivyo inamaanisha timu yoyote katika Ligi Kuu inayotaka
kununua mchezaji wa aina hiyo wanapaswa kuwanunua kwanza wamiliki wowote
wengine.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 3 Oktoba 2014
TULIMUUZA ROJO KWA SHINIKIZO - RAIS.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni