MENEJA wa klabu ya
Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa Cesc Fabregas alitaka kujiunga nao
tena kabla ya kujiunga na Chelsea. Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal
aliwahi kuitumikia timu hiyo kwa miaka nane kabla ya kuhamia Barcelona
lakini baada ya kushindwa kutamba alihamia Stamford Bridge kwa kitita
cha euri milioni 36 katika usajili wa kiangazi. Pamoja na kwenda kwa
mahsimu wao Wenger ameonyesha bado kumkubali kiungo huyo wa kimataifa wa
Hispania. Wakati akiulizwa kama Fabregas alitaka kurejea Arsenal,
Wenger alikubali na kudai kuwa pamoja na kwamba hakuzungumza naye moja
kwa moja lakini alitaarifiwa kuwa anaweza kwenda Chelsea. Wenger
aliendelea kudai kuwa wakati kiungo alipondoka kwenda Barcelona
walimnunua Mesut Ozil hivyo hawakuwa na haja ya kusajili kiungo wa
kushambulia katika usajili wa kiangazi. Pamoja na hayo Wenger amesema
bado anampenda nyota huyo na kuheshimu maamuzi yake na kudai kuwa
anastahili kupokewa kwa heshima pindi timu hizo zitakapokutana Jumapili.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 3 Oktoba 2014
FABREGAS ALITAKA KURUDI ARSENAL - WENGER.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni