MKUU wa kikosi kazi cha
kupambana na na ubaguzi wa rangi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA,
Jeffrey Webb amedai kuwa ubaguzi katika soka la Uingereza uko wazi. Webb
ubaguzi huo unaonekana kwa kukosekana kwa watu wenye asili ya kiafrika
katika nafasi muhimu katika soka la nchi hiyo. Mapema ofisa mkuu wa
Chama cha Wachezaji wa Kulipwa, Gordon Taylor alifafanua kuwa ubaguzi ni
suala lilijificha sana katika soka la nchi hiyo. Lakini kauli yake hiyo
imepingwa vikali na Webb na kudai kuwa sio la lililojificha kwani liko
wazi mbele ya macho yao na hakuna mtu anayetaka kulifanyia kazi. Webb
ambaye pia ni kiongozi wa shirikisho la soka kwa nchi za Carribean na
Amerika Kaskazini na Kati alimtolea mfano kocha wa timu ya vijana ya
Chelsea Eddie Newton. Newton mwenye umri wa miaka 42, alikuwa akifanya
kazi chini ya Roberto di Matteo wakati Chelsea walipotwaa taji la Ligi
ya Mabingwa Ulaya mwaka 2012 lakini hakufanyiwa mahojiano yoyote. Webb
amesema kwa kitendo kama hicho haoni kama ubaguzi ni suala lililojificha
kama inavyodaiwa bali liko wazi na hatua makusudi zinapaswa kuchukuliwa
ili kulitatua.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 9 Oktoba 2014
UBAGUZI WA RANGI KATIKA SOKA UINGEREZA UKO WAZI - WEBB.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni