RAIS wa AS Roma, James
Pallotta anaamini klabu hiyo ni imara zaidi kuliko mabingwa watetezi wa
Serie A Juventus. Kikosi cha Roma kinachonolewa na kocha Rudi Garcia
kilitandikwa mabao 3-2 na mabingwa hao wa Italia jijini Turin Jumapili
iliyopita lakini Pallotta anaamini kuwa utata na ugumu wa mchezo huo
unaonyesha wazi kuwa timu hizo sasa zinalingana kiviwango. Akihojiwa
Pallotta amesema kwa maono yake anadhani Roma wako imara zaidi ya
Juventus na mchezo wa uliopita umeonyesha ushahidi kamili kwenye hilo
pamoja na kwamba walipoteza. Rais huyo aliendelea kudai kuwa anajua
Juventus ni timu imara lakini wana wachezaji wa kiwango kama hicho kama
sio zaidi nab ado waliwakosa wachezaji wao muhimu kama Davide Astori,
Kevin Strootman na Daniele De Rossi. Roma kwasasa wako katika nafasi ya
pili katika msimamo wa Serie A wakiwa na alama 15 katika michezo sita
waliyocheza, wakitamnguliwa na vinara Juventus kwa tofauti ya alama
tatu.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 9 Oktoba 2014
ROMA WAKALI KULIKO JUVENTUS - PALLOTTA.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni